Arusha
Home » » RC GAMBO AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUACHA DHANA YA KUOGOPA KUSTAAFU

RC GAMBO AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUACHA DHANA YA KUOGOPA KUSTAAFU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akizungumza katika mkutano wa nane wa wadau wa mfuko wa mafao ya kustaafu wa GEPF jijini Arusha juzi ,wakati akifunga mkutano huo ambapo aliwataka wastaafu watarajiwa kujiandaa kustaafu kwa kubuni miradi mbalimbali ya kuongeza kipato hali itakayosaidia wao kujiendeleza kimaisha(Habari Picha na Pamela Mollel Arusha)

 Katibu Mkuu katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Eric Shitindi akizungumza katika mkutano huo ambapo alisema ni vyema watumishi wakajianda mapema wakiwemo wa umma na sekta binafsi


Mkurugenzi wa mfuko wa GEPF Daudi Msangi alisema kuwa tayari kuna mikakati mbalimbali ambayo imeletwa kwenye mkutano huo na itaanza kufanyiwa kazi kwa malengo ya kuboresha maslai ya wanachama na nchi kwa ujumla

Mwenyekiti wa bodi Ya wadhamini,wa mfuko huo Joyce shaidi akizungumza katika mkutano huo
 Kulia ni mkuu wa kitengo cha kusimamia amana za wawekezaji katika benki ya CRDB Bw.Masumai Ahmed
 
Wadau wa mkutano wakiwa wamesimama kuashiria kumalizika kwa mkutano huo

Mkuu wa mkoa  wa arusha Mrisho Gambo amewataka Watumishi katika sekta za umma  kuacha dhana ya kuogopa  kustaafu kazi pindi wanapofikia muda wa kustaafu badala yake wanatakiwa kujipanga kabla muda haujafika.

Aidha watumishi wanaogopa kustaafu kwa kuwa wanaanza kujiandaa miaka miwili kabla hali ambayo inawapa uoga mkubwa wastaafu watarajiwa

Mrisho Gambo ameyasema hayo jana  wakati akifunga mkutano wa mfuko wa mafao ya kustaafu (GEPF) uliokuwa ukiendelea  jijini Arusha

Gambo alisema kuwa kwa sasa wastaafu wanapata magonjwa ya moyo kwa kuwa hawajajiandaa na kubuni miradi ambayo inaweza kuwaletea vipato kama mishahara yao ilivyokuwa

Alisema maandalizi ni muimu sana kwa wafanyakazi hata kama bado hawajafikia muda wa kustaafu kwani kustaafu sio ajali bali ni kitu ambacho kipo na kimeshawekewa utaratibu na mifuko ya hifadhi jamii hapa nchini pamoja na Serikali.

"Wastaafu wengi wanakufa pindi wanapoacha kazi hiyo sio sawa ni lazima kila mtu ajiandae na abuni njia mojawapo ya kujiongezea kipato kwani hata kama ukijiajiri mwenyewe ni lazima utapata kipato kama kile ulicho kuwa unalipwa kama sehemu ya ujira wako "aliongeza Gambo.

Wakati huo huo aliwataka wakuu wa mifuko ya hifadhi hapa nchini kuhakikisha kuwa wanatoa elimu ya kujiandaa kustaafu kwa wafanyakazi wake kwani uzoefu unaonesha kuwa asilimia kubwa ya wafanyakazi hawana elimu hiyo

Alisema kama wafanyakazi watakuwa na elimu hiyo ya kustaafu basi itasaidia kupunguza  ulalamishi kwa wastaafu,magonjwa ya moyo,vifo visivyo na lazima vinavyotokea.

Naye mkurugenzi wa mfuko huo Daudi Msangi alisema kuwa tayari kuna mikakati mbalimbali ambayo imeletwa kwenye mkutano huo na itaanza kufanyiwa kazi kwa malengo ya kuboresha maslai ya wanachama na nchi kwa ujumla.
 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa